Wanasiasa waichambua Serikali ya JK 2012

Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi James Mbatia akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuunga mkono wakazi wa Mtwara kupinga usafirishaji wa gesi kwenda Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa Kampeni na Uchaguzi NCCR, Faustine Sungura


Kwa ufupi
“Matukio ya kukojolewa kwa kitabu kitakatifu (Quran), kuchomwa moto kwa baadhi ya makanisa na kuongezeka kwa vuguvugu za kidini, ni baadhi ya mambo ambayo nayaona kuwa hayakushughulikiwa ipasavyo na hili ni doa kubwa kwa utawala wa Rais Kikwete,” alisema Profesa Lipumba.

WANASIASA wametoa tathmini ya utendaji wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kwa mwaka 2012, huku wakibainisha upungufu katika maeneo kadhaa ambayo wameishauri iongeze nguvu kuyatekeleza mwaka huu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, walisema pamoja na Rais Kikwete kujisifu kwamba Serikali yake imefanikiwa mambo mengi, kuna maeneo mengi ya msingi ambayo hayakufanikiwa.
Katika salamu zake za mwaka mpya Desemba 31, 2012, Rais Kikwete alifafanua mambo mbalimbali ambayo Serikali yake ilifanikiwa kuyatekeleza mwaka uliopita kwenye sekta za elimu, afya, kilimo, nishati na gesi, miundombinu na barabara, huku akikiri pia changamoto katika maeneo kadhaa.
“Mwaka tunaoumaliza leo ulikuwa wenye mambo mengi mazuri na mafanikio makubwa, lakini ulikuwa na changamoto zake. Baadhi zilikuwa ngumu na zipo zilizokuwa za kusikitisha na kuhuzunisha,” alisema Rais Kikwete.
Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema kwamba baadhi ya maeneo Rais aliyoshindwa kuyafanikisha ni utekelezaji wa Kilimo Kwanza... “Nenda kamuulize mzazi wako, najua ni mkulima kule kijijini.
Akuelezee kama anajua chochote kuhusu Kilimo Kwanza. Wanayosema viongozi wa Serikali ni siasa tu hakuna mikakati ya kiutendaji,” alisema Dk Slaa.
“Kutofanikiwa kwa Kilimo Kwanza kunatokana na mikakati isiyo makini. Serikali iliagiza matrekta, lakini ikashindwa kuyasimamia na hata kuwajengea uwezo wananchi katika kutekeleza mbinu za mapinduzi hayo.”
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema utendaji wa Serikali mwaka jana 2012 haukuwa wa kuridhisha, ingawa kuna mwonekano wa mafanikio.
“Katika utendaji wake, hakuna alama yoyote iliyoongezeka, ameendelea (Rais) kushikilia alama ileile kama ya miaka ya nyuma. Haimaanishi kwamba amekwenda chini, hapana. Jambo la msingi ni kwamba amekuwa siyo mwepesi kusimamia mambo yake ya msingi.”
Lipumba alitaja baadhi ya mambo aliyosema kuwa yamemtia doa Rais katika utendaji wake mwaka 2012 kuwa ni polisi kuwaandama wananchi na wakati mwingine kujitokeza kwa vifo vilivyohusishwa na utendaji mbaya wa jeshi hilo.
“Vyombo vya ulinzi na usalama vilitumbukia kwenye kashfa ya matumizi mabaya ya madaraka ikiwamo kusababisha vifo vya raia, jambo ambalo linakwenda kinyume na misingi ya utawala bora.
Tumeshuhudia matukio ya raia kuuliwa kule Morogoro na tukio la kuuliwa kwa mwandishi wa habari mkoani Iringa. Jambo la kushangaza ni kwamba pamoja na matukio hayo kukithiri na Jeshi la Polisi kuwa na mikono yake, lakini hakuna hatua makini na za wazi zilizochukuliwa dhidi ya wahusika,” alisema Profesa Lipumba.
Wanasiasa waichambua Serikali ya JK 2012 Wanasiasa waichambua Serikali ya JK 2012 Reviewed by bongo qualities on 2:59 AM Rating: 5
ads 728x90 B
Powered by Blogger.